Ili ushahidi ukubalike kutumika mahakamani lazima uzingatie mambo makuu yafuatayo; a) Lazima uendane na suala lililopo katika shauri b) Lazima ushahidi huo uwe ukikubalika kisheria c) Lazima ushahidi huo utolewe na mtu anayekubalika (mwenye ruksa) ya kutoa ushahidi mahakamani. d) Lazima upatikane kwa njia halali.